Tanzania yazindua rasmi ubalozi Algeria

Serikali ya Tanzania imezindua rasmi ubalozi wake jijini Algiers, Algeria.

 

Ufunguzi huo umefanywa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Stergomena Tax na kuhudhuriwa na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Ahmed Attaf,  Balozi wa kwanza wa Algeria kuhudumu nchini Tanzania,  Noureddine Djoudi na Jumuiya ya Wanadiplomasia nchini Algeria.

Kiwango cha ubadilishaji wa biashara kati ya Tanzania na Algeria ni cha chini ikilinganishwa na fursa nyingi zilizopo. Algeria yenye eneo lake la kimkakati na uchumi inatoa fursa kubwa kwa biashara za Tanzania. 

Akihutubia kwenye ufunguzi wa ubalozi huo Waziri Tax ameeleza kuwa Tanzania na Algeria zimejizatiti kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kwa lengo la kukuza ushirikiano wenye maslahi kupitia sekta za kipaumbele kama vile sekta za kilimo, madini, utalii, mafuta na gesi, vifaa tiba, viwanda, nishati pamoja uchumi wa buluu.

Naye  Attaf ameeleza kuwa ziara ya Waziri Tax imekuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa wamepata fursa ya kuzungumza masuala ya ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji na sekta nyingine muhimu kwa maendeleo ya mataifa hayo mawili.

“Balozi zinafaa kuendelea kuwa madaraja ya muhimu kati ya watu, nchi na mataifa.  Balozi zetu zinawajibika na kukuza, kuimarisha ushirikiano na uhusiano kati ya nchi na nchi ili kuleta tija zaidi na kuziwezesha nchi zetu kunufaika kiuchumi,’’ amesema Attaf.

Ufunguzi wa Ubalozi umefanyika pembezoni mwa Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria, ambao umemalizika kwa mafanikio na kuwezesha kusainiwa kwa Hati 8 za Makubaliano ya Ushirikiano katika sekta za nishati, mafuta na gesi, elimu na teknolojia, mafunzo ya diplomasia, kumbukumbu na nyaraka, ulinzi na usalama, ushirikiano wa kidiplomasia, kilimo na afya. 

Uhusiano kati ya Algeria na Tanzania uliasisiwa mwaka 1963 mara baada ya uhuru wa Tanganyika. Tangu wakati huo nchi hizi zimeendelea kushirikiana katika maeneo mbalimbali kwa maslahi ya pande zote. Vilevile katika kuimarisha ushirikiano huo Tanzania imefanya ufunguzi wa Ubalozi wake nchini Algeria ambao ulianza kutekeleza majukumu yake tangu mwaka 2017.

Viongozi wengine waliohudhuria ufunguzi huo ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, Naibu Makatibu Wakuu kutoka Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia, Nishati na Mambo ya Ndani ya Nchi.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
John Pombe Joseph Magufuli
John Pombe Joseph Magufuli
1 month ago

uraisi MASHINDANO NANI AZIKWE KIONGOZI AU ASIYE KIONGOZI; MWEUPE AU MWEUSI

MAPINDUZIII.PNG
julizaah
julizaah
Reply to  John Pombe Joseph Magufuli
1 month ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 
.
.
Check The Details HERE….. http://www.join.salary49.com

Last edited 1 month ago by julizaah
Carol M. Wakefield
Carol M. Wakefield
Reply to  julizaah
1 month ago

Google is by and by paying $27485 to $29658 consistently for taking a shot at the web from home. I have joined this action 2 months back and I have earned $31547 in my first month from this action. I can say my life is improved completely! Take a gander at it what I do 
.
.
.
For Details►—————————➤ https://fastinccome.blogspot.com/

JennifeButtram
JennifeButtram
1 month ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 

Check The Details HERE…..  https://webonline76.blogspot.com/

Last edited 1 month ago by JennifeButtram
Umbrella (Orange Version)
Umbrella (Orange Version)
1 month ago

MASHINDANO NANI AZIKWE KIONGOZI AU ASIYE KIONGOZI; MWEUPE AU MWEUSI, MVAA VIZURI AU MVAA VIBAYA

MAPINDUZIIII.PNG
Back to top button
5
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x