TBA yapewa mwezi mmoja kukamilisha ujenzi nyumba ya jaji

Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, ametoa mwezi mmoja kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa jengo la Mheshimiwa Jaji Kanda ya Shinyanga ili aweze kuhamia na kutumia jengo hilo.

Amezungumza hayo mkoani Shinyanga mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo pamoja na jengo la Mkuu wa Wilaya ya Kishapu linalojengwa na Vikosi vya Ujenzi na kusimamiwa na Wakala huo ambapo amesisitiza Wakala huo kujenga majengo bora yatakayodumu kwa kipindi kirefu.

“Hakikisheni mnamsimamia mkandarasi ili ajenge kwa viwango hivyo hivyo vilivyopo katika usanifu”, amesisitiza Naibu Waziri huyo.

Advertisement

Awali akitoa taarifa ya miradi hiyo Kaimu Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), mkoa wa Shinyanga Eng. Nestory Nanguka, ameeleza kuwa mpaka sasa utekelezaji wa jengo la Mheshimiwa Jaji Kanda ya Shinyanga umefikia asilimia 85 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu na ujenzi wa jengo la Mkuu wa Wilaya ya Kishapu umefikia asilimia 65.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *