Viongozi washauri ushirikiano upatikanaji nishati endelevu

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko.

Viongozi mbalimbali wanaoshiriki mkutano wa kimataifa kuhusu matumizi ya nishati endelevu kwa watu wote unaofanyika Barbados wameshauri kuimarishwa kwa ushirikiano wa kikanda na kimataifa ili kuwezesha upatikanaji wa nishati endelevu kwa gharama nafuu.

Akizungumza katika mkutano huo unaofanyika mji mkuu wa nchi hiyo, Bridgetown, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko amesema Tanzania kwa upande wake chini ya uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan, imepanga kuwawezesha asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Advertisement

Amesema kupitia mradi wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) unaozalisha megawati 2,115 utawezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika na endelevu kwa maendeleo na ustawi wa wananchi katika ngazi mbalimbali.

Dk Biteko amesisitiza kuwa, utekelezaji wa lengo namba 7 katika mpango wa maendeleo ya milenia unahitaji ushirikiano miongoni mwa Serikali na sekta binafsi katika kuboresha upatikanaji wa nishati safi ikiwa ni moja ya utatuzi wa changamoto zilizopo.

Amesema ni muhimu kwa mataifa kuwekeza katika miundombinu kwa ajili ya upatikanaji wa nishati safi sambamba na kuweka mifumo ya ubunifu na utashi katika kuwezesha upatikanaji wa nishati kwa usawa bila kuacha makundi mengine.

Naye, Waziri Mkuu wa Barbados, Mia Mottley amesema ni wakati sasa wa kuweka mkakati wa kimataifa na kukubaliana kushirikiana kumaliza changamoto ya upatikanaji wa nishati kwa wote.

Akizungumzia mkutano wa misheni 300 (M300) uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Mia amesema inatia simanzi kuwa na watu zaidi ya milioni 600 barani Afrika wanaishi bila huduma ya umeme suala ambalo limesababisha changamoto katika nchi nyingi duniani.

“Tunahitaji kupata ufumbuzi wa changamoto zilizopo, uwe ufumbuzi wa ndani au kutoka katika nchi yoyote duniani,” amesema Mottley.

5 comments
    1. Can you imagine making $18,000 a month while working from home just a few hours a day? I’m doing it, and I never thought it was possible until I found this online opportunity. The work is super easy, and you don’t need any prior experience—just a desire to succeed! I can’t believe how much my life has changed in such a short time. If you’re ready to take control of your income, visit the website and get started today!

      Visit This…… http://www.worksprofit7.com/

  1. Howdy! Someone in my Facebook group shared this website with us so I came to take a look.

    I’m definitely enjoying the information. I’m
    bookmarking and will be tweeting this to my followers!
    Excellent blog and great design.

  2. Find Online Jobs (8000$-95000$ Weekly) safe and secure! Easy Acces To Information. Simple in use. All the Answers. Multiple sources combined. Fast and trusted. Discover us now! Easy & Fast, 99% Match.
    open this site ↠↠☛ 𝐖𝐰𝐰.𝐖𝐨𝐫𝐤𝐬𝐏𝐫𝐨𝐟𝐢𝐭𝟕.𝐂𝐨𝐦

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *