Wanafunzi watatu wafa kwa radi Dar

DAR ES SALAAM; Wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi Msongola wilayani Ilala, Dar es Salaam wamefariki dunia baada ya kupigwa na radi, huku wengine wawili wakijeruhiwa.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea Machi 18, 2026 majira ya saa 5:00 asubuhi katika eneo la Msongola.

Amesema waliojeruhiwa ni Nadri Maneno (8), mwanafunzi wa darasa la tatu na Mahadi Ramadhan (8), mwanafunzi wa darasa la pili, ambao wamepelekwa hospitali kwa matibabu.

Waliofariki dunia ni Alexander Paul, mwanafunzi wa darasa la tano, Ally Pongwe, mwanafunzi wa darasa la tatu na Hudhaifa Shafii, mwanafunzi wa darasa la tano.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

  2. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
    .
    This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button