Wananchi Babati waonywa vitendo viovu uchaguzi mkuu

MANYARA: Zoezi la kupiga kura kuwachagua viongozi bora ni zoezi muhimu kwa mustakabali wa taifa katika kudumisha amani na utulivu wa nchi hivyo halipaswi kuhujumiwa.
Wananchi Wilaya ya Babati mkoani Manyara wameonywa kujiepusha na matamshi au vitendo vyovyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani na utulivu wakati wa zoezi la uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu kwani ni kosa kisheria.
Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda ametoa kauli hiyo Oktoba 20, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuwa Serikali haitavumilia vitendo vyovyote vitakavyolenga kuvuruga amani wakati wa uchaguzi huo.
Amesema zikiwa zimebaki siku nane za kwenda kupiga kura Vitendo vyovyote vya kuwazuia watu wengine kwenda kupiga kura kwa kuwatisha au kushawishi ni kutenda kosa kwa mujibu wa sheria
”Awe ni mtu binafsi au kikundi cha watu ambao wanafikiri na kupanga njama za kuhujumu zoezi la uchaguzi mkuu ujao ni kosa kisheria na watachukuliwa hatua Aidha kamati ya usalama imeimarishwa katika kulinda wananchi pamoja na mali zao katika kipindi cha uchaguzi Mkuu,” ameongeza.

”Ni muhimu sana kwa kila mtanzania mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea ambaye alipata nafasi ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapigakura, kupiga kura,aweze kushiriki katika zoezi hili muhimu la Kikatiba”
Kwa kuamua kukaa nyumbani na kuwaacha watu wengine waweze kukuchagulia viongozi sio uzalendo hivyo wananchi waende wakapige kura kwa amani na utulivu, wakitumia haki yao ya kuwachagua Rais, wabunge na madiwani wanaowataka.
Kupitia Tume ya uchaguzi elimu ya mpiga kura imeendelea kutolewa maeneo ya pembezoni na mitandao ya kijamii ambapo amesema vijana wakitumia ipasavyo watapata elimu na kuwasaidia wengine.
Amesema zikiwa zimebaki siku nane za kwenda kupiga kura Vitendo vyovyote vya kuwazuia watu wengine kwenda kupiga kura kwa kuwatisha au kushawishi ni kutenda kosa kwa mujibu wa sheria
”Awe ni mtu binafsi au kikundi cha watu ambao wanafikiri na kupanga njama za kuhujumu zoezi la uchaguzi mkuu ujao ni kosa kisheria na watachukuliwa hatua aidha kamati ya usalama imeimarishwa katika kulinda wananchi pamoja na mali zao katika kipindi cha uchaguzi Mkuu.” Ameongeza
”Ni muhimu sana kwa kila mtanzania mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea ambaye alipata nafasi ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapigakura, kupiga kura,aweze kushiriki katika zoezi hili muhimu la Kikatiba”
Kwa kuamua kukaa nyumbani na kuwaacha watu wengine waweze kukuchagulia viongozi sio uzalendo hivyo wananchi waende wakapige kura kwa amani na utulivu, wakitumia haki yao ya kuwachagua Rais, wabunge na madiwani wanaowataka.
Kupitia Tume ya uchaguzi elimu ya mpiga kura imeendelea kutolewa maeneo ya pembezoni na mitandao ya kijamii ambapo amesema vijana wakitumia ipasavyo watapata elimu na kuwasaidia wengine.



