Wananchi wataka vifaa tiba zahanati Visakazi

WANANCHI wa kijiji cha Visakazi, kata ya Ubena, Halmashauri ya Chalinze, mkoani Pwani wameiomba serikali kutatua changamoto ya ukosefu wa watumishi, vifaa tiba na vitendea kazi katika zahanati ya kijiji hicho

Ombi hilo lilitolewa na Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho, Jamila Makwaya wakati akitoa taarifa ya maendeleo ya kijiji kwa kamati ya siasa ya Wilaya ya Bagamoyo katika mbio za Bendera ya chama Cha mapinduzi (CCM) zinazoendelea wilayani humo.

Alisema licha ya jengo la zahanati hiyo kukamilika kwa asilimia 100 bado kuna changamoto ya ukosefu wa vifaa tiba, vitendeakazi pamoja na kukosekana kwa watumishi.

“Zahanati hii imekamilika tangu Julai mwaka jana mpaka sasa hatujapata vifaa tiba, jengo halina vitendea kazi na watumishi ikiwemo wauguzi hatuna tunaomba serikali itusaidie kutatua changamoto hiyo.”alisema

Alisema wananchi wamekuwa wakipata adha ya kwenda mbali kwa ajili ya matibabu hali ambayo imekuwa ikieendelea kuhatarisha afya za wananchi hususani wanawake wajawazito ba watoto.

Diwani wa kata ya Ubena, Geofrey Kamugisha, alisema zahanati hiyo imegharimu zaidi ya Sh milioni 67 ambapo Serikali Kuu imetoa milioni 53, wananchi Sh milioni 13 na Halmashauri ya Chalinze Sh milioni 10.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, wilaya ya Bagamoyo, Abdurashidi Zahoro, aliagiza Halmashauri ya hiyo kuhakikisha vifaa hivyo vinafika mapema.

“Naagiza vifaa ikifika mwezi wa nane viwe vimekuja hapa ili wananchi waendelee kupata huduma ya Afya kama ilivyokusudiwa na vifaa kama vinaletwa waangalie maeneo ya pembezoni kwanza”alisema

Mbali na hilo pia aliagiza Halmashauri ya hiyo kusaidia ujenzi wa zahanati ya Kijiji Cha Mwidu kutokana na kwamba wananchi tayari kwisha changia nguvu ambapo wametoa zaidi ya milioni 27.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Hardeven
Hardeven
2 months ago

super fast money earning online job to flood the cash in your bank acc every week. from this only by working for 2 hrs a day after my college i made $17529 in my last month. i have zero experience when i joined this and in my first month i easily made $11854. so easy to do this job and regular income from this are just superb. want to join this right now? just go to this web page for more info————–>>> http://www.dailypro7.com

Kathleen D. Holloway
Kathleen D. Holloway
Reply to  Hardeven
2 months ago

Home cash earning job to earns more than $500 per day. getting paid weekly morethan $3.5k or more simply doing easy work online. no special skills requiredfor this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this byfollow details here.
.
.
Here►—————————➤ https://fastinccome.blogspot.com/

neknoyirze
neknoyirze
Reply to  Hardeven
2 months ago

svsv
I basically make about $14,000 to $18,000 a month online. It’s enough to comfortably replace my old jobs income, especially considering I only work about 10-13 hours a week from home. I was amazed how easy it was after I tried it copy below web.
.
.
Detail Are Here—————————————————>>> http://WWW.JOIN.HIRING9.COM

Last edited 2 months ago by neknoyirze
Floy King
Floy King
2 months ago

I’m using an online business opportunity I heard about and I’ve made such great money. It’s really user friendly and I’m just so happy that I found out about it. Here’s what I do.

For more details visit————————➤ https://workscoin1.pages.dev/

BerniceNickell
BerniceNickell
2 months ago

This year do not worry about money you can start a new Business and do an online job I have started a new Business and I am making over $84, 8254 per month I was started with 25 persons company now I have make a company of 200 peoples you can start a Business with a company of 10 to 50 peoples or join an online job.

For more info visit on this web Site. . . . . . . . .>>> http://www.Richcash1.com

Last edited 2 months ago by BerniceNickell
Back to top button
5
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x