Wanawake , vijana sekta ya Tehama wakumbukwa

DAR ES SALAAM: Tume ya Tehama nchini imeingia makubalino ya ushirikiano na Taasisi ya Ruge Mutahaba ushirikiano unaolenga kuwainua wanawake na vijana waliopo katika sekta ya Tehama nchini.

Hafla ya kusaini makubaliano hayo imefanyika jijini Dar es Salaam Desemba 14, 2023  na kuhudhuriwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama nchini,Dk Nkundwe Mwasaga pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Ruge Mutahaba, Cynthia Bavo.

Ushirikiano huo unalenga maeneo muhimu ya utafiti na maendeleo ikiwa ni pamoja na kutoa ujuzi kwa vijana na wanawake lakini pia kusambaza uelewa  juu ya masuala ya Tehama kwa wanawake na vijana waliopo katika sekta ya Tehama.

Advertisement

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *