Wapongeza ujenzi mradi wa maji Mbinga

Wapongeza ujenzi mradi wa maji Mbinga

WAKAZI wa Kijiji cha Ruvumachini Halmashauri ya Mji Mbinga mkoani Ruvuma, wameishukuru serikali kwa kuanza ujenzi wa mradi mkubwa wa maji utakaomaliza kero ya muda mrefu ya maji  safi na salama katika kijiji hicho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mbele ya Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Kanali Laban Thomas, walisema, tangu serikali  ilipoanza kujenga  mradi huo, wana matumaini makubwa ya kuishi na kuwa na maisha bora na kuondokana na mateso makubwa yanayosababishwa na ukosefu wa maji ya bomba.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Hagapi Komba, alisema, changamoto ya maji katika kijiji hicho ni kubwa na ya muda mrefu hali iliyosababisha baadhi ya watumishi wa serikali wanaopelekwa kufanya kazi, wakiwemo walimu wa shule ya msingi kuomba uhamisho kwenda shule nyingine na wengine kukimbia, ili kuepuka kero ya maji.

Advertisement

Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mbinga, Mhandisi Mashaka Sinkara )kushoto), akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Ruvumachini wilayani humo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Laban Thomas.(Picha zote na Muhidin Amri).

Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini, Jonas Mbunda, alisema, uamuzi wa serikali  kutoa kiasi cha Sh bilioni 1.3, kwa ajili ya kutekeleza mradi huo  imethibitisha uaminifu wake kwa wananchi wa jimbo hilo na kudhihirisha  kauli mbiu ya kumtua mama ndoo kichwani.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa, Kanali Laban Thomas, ameuagiza Wakala wa Maji Safi na Usafi  wa Mazingira (Ruwasa), Mkoa wa Ruvuma, kuhakikisha inamsimamia mkandarasi anayejenga mradi huo, ili akamilishe kazi kwa wakati na ubora wa hali ya juu.

Pia amewataka amewataka wananchi wa kutunza mradi huo pamoja na vyanzo vya maji.

 

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *