Wizara ya Afya yapigwa jeki vita dhidi ya malaria

DAR ES SALAAM; WIZARA ya Afya nchini imepokea msaada wa vifaa vya maabara hadubini ‘Microscope’ 133 kutoka kwa Serikali ya Marekani kupitia Shirika lao la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) na Mpango wa Rais wa Marekani wa Kupambana na Malaria (PMI).

Akizungumza leo Novemba 14, 2023 Mkurugenzi wa Ofisi ya Afya kutoka USAID Tanzania, Anne Murphy amesema kuwa hadubini hizo 133 zitasambazwa katika vyuo vya kati vinavyosimamiwa na Wizara ya Afya pamoja na Taasisi za Tafiti.

Amesema lengo ni kusaidia kuimarisha uwezo wa wataalamu wa maabara nchini katika upimaji wa vimelea vya malaria kwa ufanisi.

Vifaa hivyo vina thamani ya zaidi ya Dola za Marekani 448,000 sawa na Sh bilioni 1.2 ambapo vitasambazwa katika vyuo vya kati ambavyo vipo kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya, Morogoro, Tanga, Mara na Singida, ili kusaidia upimaji wa vimelea vya Malaria na magonjwa mengine kwa ufanisi zaidi ikiwa ni mpango wa kupambana na ugonjwa huo.

Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUCOHAS) kimekabidhiwa hadubini 12 kwa niaba ya vyuo vilivyopo chini ya Wizara ya Afya vinavyotoa mafunzo ya kozi ya maabara vilivyopo katika mikoa hiyo sita.

Amesema kuwa hadubini hizo na vitendanishi vingine vya maabara vilivyotolewa vitawezesha Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria kuimariasha uwezo wa kimaabara katika uchunguzi na kusaidia utoaji matibabu ipasavyo hivyo kusaidia kuokoa maisha ya watu na kuzuia madhara ya malaria.

Ameipongeza Tanzania kupitia Wizara ya Afya kwa juhudi kubwa za kupambana na kuhakikisha kiwango cha malaria kinashuka nchini kutoka asilimia 14 mwaka 2015 mpaka asilimia 8 mwaka 2022.

Awali akitoa salamu za ufunguzi , Mkurugenzi wa Hospitali ya Muhimbili Profesa Mohamed Janabi ameishukuru Marekani kwa msaada huo uliolenga kusaidia kuendelea kupambana na kuutokomeza ugonjwa wa malaria nchini.`

“Malaria ni tatizo kubwa linauwa watu 500,000 kila mwaka na bahati mbaya asilimia 96 ya vifo hivyo vinatokea Afrika, takwimu za mwaka jana kila baada ya dakika mbili kuna mtoto mmoja Afrika anafariki kwa ajili ya malaria,”amesema Janabi na kuongeza

“Ni tatizo kubwa, hivyo vifaa hivi vitatusaidia kwa wanafunzi wetu hapa kusoma kwa kina na wakitoka hapa wanakua wabobezi na ndio watakuwa wataalamu wa afya katika vituo vya afya, naishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuhimarisha uhusiano na mataifa ya nje ambao leo wametuletea msaada huu mkubwa.

Amesema msaada huo umekuja wakati muafaka kipindi ambacho serikali kupitia Wizara ya Afya imewekeza fedha nyingi ili kuboresha huduma za afya nchini kwa kununua dawa na vifaa tiba.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
EmmaJones
EmmaJones
25 days ago

Making extra salary every month from house more than $15,000 just by doing simple copy and paste like online job. I have received $18,000 from this easy home job. Everybody can now makes extra cash online easily.
.
.
By Just Follow———————————————————>>>  http://Www.BizWork1.Com

Angila
Angila
25 days ago

Making every month extra dollars by doing an easy job Online. Last month i have earned and received $18539 from this home based job just by giving this only mine 2 hrs a day. Easy to do work even a child can get this and start making money Online. Get this today by follow instructions
.
.
.
On This Website……………..> > http://remarkableincome09.blogspot.com

Scholarship ya Mwanadamu mwenye
Scholarship ya Mwanadamu mwenye
24 days ago

Scholarship ya Mwanadamu mwenye akili ya ‘Kinyonga mdogo zaidi duniani’ aliyegundulika Tanzania

Kinyonga kwa jina Brookesia urefu wake ni milimita 13.5

Wanasayansi wanaamini kuwa wamebaini kinyonga mdogo zaidi duniani ambaye ukubwa wake ni sawa na mbegu.

Vinyonga hao wawili ilibainika nchini Madagasca na timu ya sayanasi ya Ujerumani na Madagasca.

Kinyonga wa kiume aliyepewa jina la Brookesia urefu wake ni milimita 13.5.
Na kinyonga huyo anakuwa mdogo zaidi kati ya spishi karibu 11,500 za vinyonga, kulingana na rekodi ya hifadhi ya wanyama ya taifa ya Bavaria katika mjini mkuu wa Munich.

Urefu wake kutoka juu hadi chini ni milimita 22.
Kinyonga wa kike ni mkubwa kidogo takribani milimita 29, taasisi hiyo imesema, ikiongeza kwamba aina nyingine bado hazijapatikana, licha ya kwamba “juhudi zimekuwa zikiendelea”.

“Kinyonga huyo mpya aliyepatikana kaskazini mwa Madagascar eneo la msitu linalopokea mvua kubwa, huenda yuko katika hatari ya kutoweka,” kulingana na jarida la wanasayansi.

Oliver Hawlitschek, mwanasayansi wa kituo historia huko Hamburg, alisema: “Kwa bahati mbaya eneo alilokuwa akiishi mjusi huyo lilianza kuingiliwa na binadamu lakini likaanza kulindwa hivi karibuni, kwahiyo anawezaa kunusurika.”

Watafiti walibaini kwamba kinyonga huyo alikuwa anatafuta mchwa katika msitu wenye mvua kubwa na kujificha dhidi ya wanyama wala nyama usiku kwenye nyasi.
Katika msitu ambao mjusi Brookesia alipatikana umepakana na misitu mingine kaskazini mwa kisiwa, walisema.

Katika ripoti yao, wanasayansi wamependekeza kuwa kinyonga huyo aorodheshwe kama mnyama aliye hatarini katika orodha ya Shirika la IUCN, linalochunguza hali ya maelfu ya jamii za wanyama kumsaidia kumlinda na makazi yake.

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x