Zungu ndiye Spika wa Bunge

DODOMA : BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemchagua Mussa Azzan Zungu kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupata kura 378 kati ya kura 383 zilizopigwa leo mjini Dodoma.
Matokeo hayo yamethibitishwa na wasimamizi wa uchaguzi mara baada ya zoezi la kuhesabu kura kukamilika. Wagombea wengine walioshiriki katika kinyang’anyiro hicho ni Chrisant Ndege wa Chama cha Democratic Party (DP), Veronica Charles wa NRA, na Amin Alfred wa ADC, ambao kila mmoja alipata kura sifuri.
Aidha, Anita Halfan Mgaya wa NLD na Ndonge Said Ndonge walipata kura moja kila mmoja, huku kura tatu zikiharibika. Kwa ushindi huo, Zungu anachukua rasmi nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi kijacho cha uongozi. SOMA: Ndege Aahidi Bunge la Maendeleo




Nowadays earning money online is very easy . Eanrs every month online more than $17k by doing very easy home based job in part time u can also do this simple online Job by visiting websiteMore Details For Us→→ http://www.job40.media