Real Madrid yamtetea Zidane

MABINGWA wa kihistoria wa Ulaya Real MadridΒ wamesikitishwa na kauli isiyo ya kiungwana na iliyotafisiriwa kumkosea heshima ya Rais wa Shirikisho la soka la Ufaransa,Β Noel Le Graet, kumhusu Zinedine Zidane.

Baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Dunia nchini Qatar ziliibuka tetesi kuwa kiungo wa zamani wa Real Madrid na Ufaransa, Zinedine Zidane kuwa angeweza kuwa kocha wa Ufaransa au Brazil.

Tetesi za kuhusishwa na kuifundisha Brazil, Rais Noel Le Graet hakupendezeshwa nayo na aliposikia taarifa hizo alisema Β β€œπ’π’Šπ’…π’‚π’π’† π’Œπ’–π’˜π’‚ π’Œπ’π’„π’‰π’‚ π’˜π’‚ π‘©π’“π’‚π’›π’Šπ’?Β π‘―π’‚π’Šπ’π’Šπ’”π’•π’–π’Š 𝒉𝒂𝒕𝒂 π’Œπ’Šπ’…π’π’ˆπ’, π’‚π’π’‚π’˜π’†π’›π’‚ π’Œπ’˜π’†π’π’…π’‚ π’Œπ’π’Œπ’π’•π’† π’‚π’π’‚π’Œπ’π’•π’‚π’Œπ’‚! π‘°π’˜π’† π’π’ˆπ’‚π’›π’Š π’šπ’‚ π’Œπ’π’‚π’ƒπ’– 𝒂𝒖 π’π’ˆπ’‚π’›π’Š π’šπ’‚ π’•π’Šπ’Žπ’– π’šπ’‚ π’•π’‚π’Šπ’‡π’‚, π’”π’Šπ’‚π’Žπ’Šπ’π’Š π’Œπ’‚π’•π’Šπ’Œπ’‚ 𝒄𝒉𝒐𝒄𝒉𝒐𝒕𝒆 π’Œπ’Šπ’π’‚π’„π’‰π’π’π’•π’Šπ’‚ π’”π’‰π’‚π’Œπ’‚.

β€œπ‘¨π’π’Šπ’˜π’‚π’‰π’Š π’Œπ’–π’˜π’‚π’”π’Šπ’π’Šπ’‚π’π’‚ 𝒏𝒂 π’Žπ’Šπ’Žπ’Š π’‚π’˜π’† π’Œπ’π’„π’‰π’‚ π’˜π’‚ π’•π’Šπ’Žπ’– π’šπ’‚ π’•π’‚π’Šπ’‡π’‚? 𝑯𝒂𝒑𝒂𝒏𝒂, 𝒏𝒂 π’π’Šπ’”π’Šπ’π’ˆπ’†π’‘π’π’Œπ’†π’‚ 𝒉𝒂𝒕𝒂 π’”π’Šπ’Žπ’– π’šπ’‚π’Œπ’†.” aliongeza

Katika taarifa yao Real Madrid wameandika.

β€œZinedine Zidane,Β bingwa wa dunia na bingwa wa Ulaya akipigania jezi ya taifa lake, pamoja na mataji mengine mengi, anawakilisha tunu za mchezo huu na amethibitisha hilo katika maisha yake yote ya soka, kama mchezaji na kama kocha.”

β€œKauli ya Rais wa Shirikisho la soka Ufaransa haikubaliki hasa kwa mtu anayebeba uwakilishi kama wake, na inamdhalilisha mwenyewe, ukirejea pia alishawahi kutoa kauli kama hizo kwa nahodha wetu Karim Benzema, mshindi wa sasa wa Ballon d’Or, Ligi ya mataifa ya Ulaya akiwa na Ufaransa mwaka 2021 na mshindi mara tano wa ligi ya mabingwa Ulaya pamoja na mataji mengine mengi.”

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button