Kabudi asifu vyombo vya habari utulivu nchini
SERIKALI imepongeza kazi iliyofanywa na vyombo vya habari nchini katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu hadi sasa.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi amesema vyombo hivyo vimekuwa vikiripoti taarifa kwa umahiri na weledi.
Profesa Kabudi alisema hayo katika mkutano wa Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba mkoani Dar es Salaam na akasema vyombo vya habari ni wadau kwa kuwa vimekuwa na utulivu nchini.
SOMA: Prof. Kabudi: AI si tishio la ajira zenu
“Vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti kwa kutambua kwamba nchi hii ni yetu na hata sisi pia,” alisema.
Profesa Kabudi alisema vyombo vya habari vimefanya kazi ya kuhakikisha kuna utulivu miongoni mwa Watanzania hasa katika kipindi cha kampeni, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.
Awali, alisema Dk Mwigulu amekuwa rafiki na mdau wa vyombo vya habari na wanahabari wote kwa ujumla na ndio maana aliwapa kundi la wahariri kipaumbele cha mwanzo kati ya makundi mengine ya kimkakati.
“Na hii imejidhihirisha kwamba miongoni mwa makundi ya mwanzo ya kimkakati ambayo umeamua kukutana nayo ni wahariri, maana yake umeona ni kundi muhimu, la wadau na marafiki zako ambao umekuwa nao katika nyakati zote na hata sasa umeendelea kuwa nalo,” alisema Profesa Kabudi.
Katika hatua nyingine, Profesa Kabudi alisema hatua kadhaa zimechukuliwa kuhusu vyombo vya habari ikiwemo sheria ya huduma za habari imefanyiwa marekebisho na imeanza kufanya kazi na bado wanaendelea kuona maeneo yatakayotakiwa kufanyiwa kazi zaidi.
Pia, alisema imeundwa Bodi ya Ithibati ya waandishi wa habari na inafanya kazi na hadi sasa waandishi 3,200 wamepewa ithibati na kutambuliwa kufanya kazi hiyo ya kitaaluma.
Alisisitiza bodi hiyo imeundwa si kuwa chombo tu cha kudhibiti bali pia cha kulea na kukuza taaluma ya habari, akiwemo yeye kwani pamoja na kwenda kusoma sheria bado ameendelea kuwa mwandishi wa habari siku zote.




Akaunti yangu ya Bank Anayo kwa breaking news zako
https://youtube.com/shorts/yIS-tRKudlg?si=DX5NtyVjbrghvKOV
JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com
Akaunti yangu ya Bank Anayo kwa breaking news zako
https://youtube.com/shorts/yIS-tRKudlg?si=DX5NtyVjbrghvKOV