Kihongosi aanza ziara Singida

SINGIDA; Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amewasili wilayani Manyoni leo Januari 18, 2026 na kupokelewa na wanachama wa chama hicho, ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi mkoani Singida.

Hiyo ni ziara maalumu inayolenga kuhakikisha chama hicho kinawafikia wanachama wote nchini sambamba na kusikiliza kero za wananchi, kuzifanyia kazi na kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Akizungumza na wanachama walio itokeza, Kihongosi aliwasilisha salamu za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan. Na aAlisisitiza umuhimu wa umoja, mshikamano na upendo.

