SELF yawaita Watanzania fursa uwekezaji

MFUKO wa Fedha wa SELF uliopo chini ya Wizara ya Fedha umewataka Watanzania kujitokeza viwanja vya Bombadia mkoani Singida Ili kufahamu fursa za uwekezaji za kifedha chini ya mfuko huo.

SOMA: Wananchi Mtwara watakiwa kuchangamkia fursa 

Wito huo umetolewa na Linda Mshana ambaye ni Meneja Masoko na Uhamasishaji wa mfuko huo akiwa kwenye maonesho ya saba ya mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Advertisement

Programu hiyo inahusisha Kanda ya Kati mikoa ya Dodoma, Shinyanga, Tabora, Manyara Dar-es-Salaam na wenyeji Singida yanayoendelea viwanja vya Bombadia Singida.

SOMA: Wanafunzi DIT kupata fursa