Serikali yaita mapendekezo kupunguza gharama za matibabu

SERIKALI imeagizwa iwasilishwe mapendekezo kuhusu namna ya kupunguza gharama za matibabu kwa wananchi.

Akizungumza na watumishi wa umma wakati akifanya majumuisho ya ziara yake mkoani Kilimanjaro, Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ametoa agizo kwa Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kukaa pamoja na kujadiliana ili kupata mapendekezo ya namna bora ya kupunguza gharama za huduma za afya kwa wananchi.

“Kote tulikopita kumekuwa na malalamiko kuhusu gharama katika sekta ya afya. Tengenezeni mapendekezo, kaeni na wenzetu wa TAMISEMI, watumeni makatibu wakuu wakae na kuandaa pendekezo litakalowasilishwa serikalini,” alisema.

Dk. Nchemba amesema kuna familia ambazo kupata Sh 20,000 au Sh 40,000 ni jambo gumu, hivyo endapo kiasi hicho kitatumika kwa ajili ya kumuona daktari pekee, baadhi ya familia hazitaweza kumudu gharama hizo. SOMA: Watu 600 wapata huduma za kibingwa utalii wa matibabu

Amesema kuwa malalamiko ya wananchi yanaonyesha kuwa mgonjwa anapofika hospitalini hulazimika kulipia kufungua faili, kumuona daktari na kufanya vipimo, hali inayosababisha kumaliza fedha zake zote kabla hata ya kupata matibabu kamili.

“Ukiwasikiliza wananchi, utaona kuwa mtu anapofika hospitalini akiwa mgonjwa anaambiwa afungue faili kwa malipo, kumuona daktari alipie, vipimo alipie, na anapogundulika na tatizo tayari fedha zimekwisha. Hali hii haimsaidii sana mwananchi. Hivyo, leteni mapendekezo ili tuishauri serikali namna sahihi ya kushughulikia suala hili,” alisema.

Aidha, amewahakikishia wananchi katika maeneo aliyoyatembelea kuwa serikali itatoa kauli kuhusu kupunguza gharama za matibabu mara baada ya mapendekezo hayo kuwasilishwa na kufanyiwa kazi. “Nafahamu kuwa tupo katika mchakato wa kuhama kutoka utaratibu tuliouzoea kwenda kwenye mfumo wa Bima ya Afya kwa Wote. Tutaliangalia suala hili na tutatoa kauli baada ya kujipanga vizuri ndani ya serikali,” alisema.

Habari Zifananazo

4 Comments

  1. I get paid over 220 Dollars per hour working from home with 2 kids at home. i never thought i’d be able to do it but my best friend earns over 15k a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life. This is what I do, check it out by Visiting Following Website……….

    HERE→→→→→→→→→→ http://Www.Work27.Info

    1. I get paid over (90$ to 200$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $18000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
      .
      HERE——————————————⊃⫸ https://Www.Cash54.Com

    2. I get paid over 220 Dollars per hour working from home with 2 kids at home. i never thought i’d be able to do it but my best friend earns over 15k a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life. This is what I do, check it out by Visiting Following Website…

      .
      M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com

  2. Start now generating extra home based cash by doing very easy and simple job from home. Last month i have earned $19753 from this job in my part time. This job is just awesome and its earning are greater than 9 to 5 office job. Join this right now by follow instructions here…

    >>>>>>>>>> http://www.giftpay7.vip

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button