Simba kwenda Misri dhidi ya Tai wa kijani

QATAR: MWAKILISHI pekee Tanzania wa michuano ya Kimataifa, Simba itamenyana na Al Masry hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Simba wataanzania ugenini nchini Misri dhidi ya Al Masry ( Tai wa Kijani) mchezo utakaochezwa kati ya April 1 au 2 na 8 /9 watarudiana katika dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
SOMA ZAIDI: Usiseme Simba! Sema mwakilishi wetu
Wekundu hao wa Msimbazi wakifanikiwa kuvuka hatua ya hiyo wanaenda kucheza nusu fainali kati mshindi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini dhidi ya Zamalek ya Misri.
Simba imefuzu hatua ya robo fainali ya kombe la Shirikisho Afrika ikimaliza kinara wa kundi A, kwa kuvuna alama 13 mbele ya CS Constantine ya Algeria iliyomaliza nafasi ya pili alama 12.



