TCRA yahimiza umakini kulinda amani, umoja

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema ni muhimu vyombo vya habari na wananchi walinde umoja, amani na mshikamano wa taifa, kwa kuzuia maudhui yasiyofaa kwa jamii.

Akiwa Dar es Salaam, Meneja wa Kitengo cha Huduma za Utangazaji TCRA, Andrew Kisaka amesema ni muhimu wananchi wafute taarifa za kizushi na wajiepushe kuzisambaza.

Kisaka amesema kumekuwa na watu wanaosambaza taarifa za kizushi mtandaoni, hasa zinazoweza kuchochea taharuki na kuvuruga amani.

Amehimiza watangazaji wazingatie kanuni za utangazaji zinazohusu kampeni za siasa wakati wa Uchaguzi Mkuu kwa kupata taarifa kwenye vyanzo rasmi na kuzingatia mizania kabla ya kutangaza au kusambaza habari hizo.

SOMA: TCRA waanzisha kampeni ulinzi mitandaoni

Kisaka amesema Kampeni ya TCRA ya ‘Futa Delete Kabi sa’ inamuwezesha mwananchi kuepuka madhara ya kuchukuliwa hatua za kisheria yanayotokana na kusambaza taarifa potofu.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma TCRA, Rolf Kibaja amesema kwa sasa kuna usambazaji wa taarifa za uzushi zinazotengenezwa kwa kutumia akili unde.

“Unaweza kutumia teknolojia saidizi kubaini uhalisia wa taarifa ya picha, ikiwemo uchapaji wake wa mara ya kwanza au kwa kuangalia viashiria kama vile takwimu zisizo sahihi, makosa ya kisarufi au majina na kuwa na vihisishi vingi vyenye kuongeza chumvi,” amesema Kibaja.

Ofisa Mhifadhi Mwandamizi wa TCRA, Raphael Mwango amesema kizazi cha sasa kinafikiwa na taarifa kwa haraka, tofauti na zamani.

Mwango amesema vijana wengi huanza kutumia simu janja mapema, hali inayowapa fursa ya kupata taarifa nzuri na potofu.

Amesema kampeni ya TCRA ni jibu la kimkakati kukabili changamoto za taarifa potofu, huku ikilenga kuwasaidia vijana na wazazi kujilinda kisheria.

Mwango amesema uzushi unaweza kuathiri afya ya akili, kuvuruga mshikamano wa wananchi, kuharibu heshima ya mtu au hata kuchangia vifo.

Amesema kampeni hio itatekelezwa kwa muda wa miezi sita na akasema TCRA imejipanga kukabili changamoto hiyo kwa kuwahamasisha wananchi kutumia teknolojia kwa uangalifu na kufuata taratibu zilizo sahihi.

Ametoa mwito kwa wananchi wawe makini na taarifa wanazopokea au kusambaza mtandaoni na akasema taarifa kuhusu matokeo ya uchaguzi zisizotolewa na mamlaka zinaweza kusababisha migogoro na taharuki isiyo ya lazima.

Habari Zifananazo

5 Comments

  1. Google pays $220 an hour online. My close relative had been unemployed for nine months, but last month, she received a $25k paycheck by working from home for 10 hours a day. Everyone should try this job now—just use this link. COPY THIS →→→→ ­­­W­­w­­w­­.S­­a­­l­­a­­r­­y­­­7­­­.­­­Z­­­o­­­n­­­e­­­

    1. I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
      .
      HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

    2. Earn cash with a job that lets you make more than $700 per day. Get paid weekly with earnings of $3,500 or more by simply doing easy online work. No special skills are required, and the regular earnings are amazing. All you need is just 2 hours a day for this job, and the income is fantastic. Anyone can get started by following the details here:

      COPY THIS →→→→ http://Www.Work99.Site

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  3. I get paid more than $100 to $500 per hour for working online. I heard about this job 3 months ago and after joining this I have earned easily 💵$20k from this without having online working skills . Simply give it a shot on the accompanying site…

    Here is I started.→→→→→→→→→ https://Www.Works6.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button