Waendesha baiskeli 200 kumuenzi Nyerere

DAR ES SALAAM :ZAIDI ya waendesha baiskeli 200 kutoka nchi mbalimbali kushiriki msafara wa Twende Butiama kumuenzi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar-es-salaam, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano kutoka kampuni ya simu ya Vodacom, Zuweina Farah amesema Kampuni ya Vodacom na taasisi zake zinalengo moja kwa jamii ikiwa ni Elimu bora , afya na kuwawezesha wajasiriamali wadogo kuwainua kiuchumi.

Amesema katika mpango wa miaka mitano ijayo wamelenga kuzisaidia shule katika  mikoa 12 hadi14.

Advertisement

DAR ES SALAAM :ZAIDI ya waendesha baiskeli 200 kutoka nchi mbalimbali kushiriki msafara wa Twende Butiama kumuenzi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere .

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar-es-salaam, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano kutoka kampuni ya simu ya Vodacom, Zuweina Farah amesema Kampuni ya Vodacom na taasisi zake zinalengo moja kwa jamii ikiwa ni Elimu bora , afya na kuwawezesha wajasiriamali wadogo kuwainua kiuchumi.

Kwa upande wake Mkuu wa Msafara wa Twende Butiama Gabriel Landa amesema msafara huo utamuenzi Baba wa Taifa kwa vitendo  kwa kupambana na maadui wa maendeleo  ambao ni ujinga, umaskini na maradhi

Amesema msafara huo uutashirikisha  watanzania wengine kuadhimisha kumbukizi ya kifo cha miaka 25 cha Baba wa Taifa tangu alipofariki

SOMA: Taasisi yaenzi miaka 101 ya Nyerere

Msafara huu utahusisha kilomita 1,846 kutokea Dar es salaam hadi Butiama huku wakitegemea kupata washiriki kutoka  maeneo mbalimbali ya Tanzania nan chi zingine kama Zimbabwe,Afrika Kusini, Namibia lengo kuwaleta pamoja watanzania na waafrika katika kuishi maono ya Hayati  Baba wa Taifa  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.