Watu 18 wanaswa kwa makosa mbalimbali Shinyanga

JESHI la Polisi mkoani Shinyanga limefanikiwa kukamata watu 81  kwa kuhutumiwa makosa mbalimbali katika kipindi cha kuanzia mwezi Novemba hadi Desemba mwaka huu.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, Janeth Magomi amesema hayo leo mbele ya waandishi wa habari nakueleza kuanza oparesheni hiyo iliyokuwa na lengo  la kubaini na kuzuia uhalifu .

Kamanda Magomi amesema watu hao licha ya kukamatwa kwa kutuhumiwa kwa makosa  wapo waliokutwa na madini ya dhahabu  bandia gramu 250, bangi gramu 9000, mirungi bunda tisa pamoja na pombe ya Moshi lita 113.

Advertisement

Kamanda Magomi amesema polisi waliokuwa doria  walifanikiwa  kukamata silaha aina ya Gobore  katika kijiji cha Bugomba A kata ya Ulewe Halmashauri ya Ushetu.

“Gobore hilo lilikuwa limepakizwa kwenye baiskeli na mtu ambaye  alikuwa akiendesha alitelekeza nakufanikiwa kukimbia lakini wanaendelea kumtafuta mtuhumiwa,” amesema Magomi.

Kamanda Magomi alisema  kesi 18 zimepata mafanikio  ambapo watuhumiwa  wanne wamefungwa  maisha huku kesi moja ya ubakaji mshtakiwa  alihukumiwa  miaka 30 kwenda  jela.

Kamanda Magomi amesema  wamefanikiwa kukamata makosa  5,376 ya usalama barabarani  ikiwa makosa ya kwenye magari ni 3,767 na makosa ya bajaji  na pikipiki ni 1,609.

“Tumefanya mikutano 97 ya utoaji elimu  juu ya kuzuia uhalifu na kuondoa ukatili  kupitia vyombo vya habari tukiwataka  wananchi kushirikiana na jeshi hili,” amesema Magomi